Teknolojia ya AI ya China yapata umaarufu nchini Kenya
Miundo ya Akili Bandia ya China (Al) inapata umaarufu miongoni mwa waendelezaji programu na makampuni ya teknolojia ya Kenya kutokana na sifa zake za gharama nafuu, utendaji wenye ushindani na kuwa Chanzo Huria, ikitoa chaguo la kuvutia kwa soko linalohitaji masuluhisho ya Akili Bandia yenye gharama nafuu na yanayokidhi mahitaji ya kienyeji. Uchambuzi wa hivi…
UM waonyesha wasiwasi kuhusu vurugu nchini Sudan
Umoja wa Mataifa umeonyesha wasiwasi kuhusu kuibuka kwa mapigano mapya nchini Sudan, ukisema mapigano hayo yanawaweka raia katika hatari kubwa na kuwafanya watu wengi zaidi kukimbia makazi yao. Mkoa wa Blue Nile umerekodi moja ya idadi kubwa ya watu wanaokimbia makazi yao, huku mamlaka za huko zikisema karibu watu 22,000 huenda wamekimbilia eneo la Gisan…
Handaki la kujikinga na mashambulizi ya anga huko Hangzhou yageuzwa kuwa “chumba chenye kiyoyozi cha asili”.
Watu wengi wanajiburudisha katika eneo la kupumzika lenye baridi huko Sipailou mjini Hangzhou mkoani Zhejiang,China. Eneo hilo limejengwa ndani ya handaki la kujikinga na mashambulizi ya anga, na ni kama “chumba chenye kiyoyozi cha asili” ambapo hali ya joto inadumishwa karibu nyuzijoto 25. Pia kumewekwa chumba cha kusoma vitabu,eneo la kucheza ping-pong, na viti 400…
Mgomo wa wafanyakazi wavuruga safari za anga nchini Kenya
Mgomo wa wafanyakazi wa anga ulioanza jumapili iliyopita nchini Kenya umesababisha shughuli za usafiri kuvurugika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) nchini humo kwa siku ya pili jana Jumatatu, huku maelfu ya wasafiri wakilalamikia kuahirishwa kwa safari zao au nyingine kukwama wasijue tarehe halisi ya safari zao. Jumapili iliyopita, Mamlaka ya…
Ethiopia yarejesha nyumbani karibu raia 100,000 kutoka nje ya nchi mwaka jana
Serikali ya Ethiopia imetangaza kuwa imewarejesha nyumbani karibu raia 100,000 waliokabiliwa na hali mbaya nje ya nchi katika miezi 12 iliyopita chini ya mpango unaoendelea unaoongozwa na serikali. Wizara ya Wanawake na Masuala ya Jamii ya Ethiopia imesema katika taarifa yake kuwa zaidi ya Waethiopia 98,900 walirudishwa nyumbani salama wakati wa duru ya hivi karibuni…
DRC yarekodi kesi zaidi ya 6,000 zilizothibitishwa za Ebola
Takwimu zilizotolewa jana zimeonesha kuwa, kesi zilizothibitishwa kuwa na maambukizi ya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) zimezidi 6,000, huku karibu vifo 3,000 vikihusishwa na ugonjwa huo. Mamlaka za huko zimeripoti kuwa, mpaka kufikia jumamosi iliyopita, DRC ilirekodi kesi 6,041 zilizothibitishwa kuwa na maambukizi ya Ebola katika mikoa sita, ikiwemo vifo 2,911, na…
Maandalizi ya Maonyesho ya Kimataifa ya Biashara ya Huduma ya China ya 2026 yakamilika
Maandalizi ya Maonyesho ya Kimataifa ya Biashara ya Huduma za China CIFTIS ya 2026 yatafanyika kuanzia tarehe 9 hadi 13 mwezi Septemba katika Hifadhi ya Shougang mjini Beijing yamekamilika. Kwa mara ya kwanza, maonyesho ya mwaka huu yataangazia eneo la maonyesho la “Huduma za China” katika eneo kuu la maonyesho, ikionyesha mafanikio bunifu na mifano…
Kampuni za Sharpa na DQ zashirikiana kuanzisha mkahawa wa ice cream unaoendeshwa na roboti
Mkahawa wa kwanza wa ice cream unaoendeshwa na roboti ulioanzishwa kwa ushirikiano wa kampuni maarufu ya ice cream Dairy Queen na kampuni ya roboti za AI ya Sharpa, umefunguliwa rasmi Agosti 29, 2026, katika Mtaa wa Wujiang, mjini Shanghai,China. Habari zinasema, mkahawa huo ni wa kwanza unaojiendesha kikamilifu, na unaofanya kazi mwaka mzima bila mapumziko….
Juhudi za uokoaji baada ya ajali ya maporomoko ya matope Xizang zaimarishwa huku idadi ya vifo ikiongezeka hadi 16
Waokoaji wanaendelea na juhudi za kuwatafuta manusura baada ya maporomoko makubwa ya matope, yaliyosababishwa na maporomoko ya barafu huko Nepal, kugonga forodha ya mpakani ya Gyirong Mkoani Xizang. Serikali ya mkoa huo imesema janga hilo lililotokea Agosti 26, limesababisha vifo vya watu 16, na wengine 546 bado hawajulikani walipo. Licha ya changamoto ya miinuko mirefu,…
DR Congo yazindua chanjo ya Ebola chini ya mfumo wa matumizi kwa watu walio hatarini
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Alhamisi ilizindua chanjo ya Ebola ya Ervebo chini ya mfumo wa matumizi kwa watu walio hatarini katika jimbo la kaskazini mashariki mwa Tshopo, huku nchi hiyo ikiongeza juhudi za kudhibiti mlipuko unaoendelea wa virusi vya Ebola vya Bundibugyo. Waziri wa Afya wa DRC Roger Kamba alizindua rasmi chanjo hiyo…