UM wasema kutakuwa na El Niño kubwa zaidi hadi Februari 2027
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), António Guterres, ameonya dunia imeingia katika eneo hatari la hali mbaya ya hewa, huku athari za El Niño zikianza kuhisiwa duniani kote. Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), limetoa takwimu za hivi karibuni kuhusu hali mbaya zaidi ya hewa kwa zaidi ya miaka 70 ambayo huenda ikaendelea…
Kenya yataka kushirikiana na China ili kuboresha viwanda vyake
Kenya inapanga kuimarisha ushirikiano na China ili kuboresha uwezo wake wa uzalishaji viwandani, kuongeza mauzo ya nje ya bidhaa zenye thamani, na kuleta nafasi za ajira kwa vijana. Maofisa kadhaa wa Kenya walisema hayo jana Alhamisi kwenye Maonyesho ya 9 ya Kimataifa ya Viwanda ya Kenya mjini Nairobi. Mkurugenzi wa taifa wa Chama cha Biashara…
Rais wa Sudan Kusini aridhia marekebisho ya katiba
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir ameridhia marekebisho ya katiba yanayoondoa hitaji la katiba ya kudumu na mwafaka wa kitaifa kukamilika kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu. Bunge la Mpito la Kitaifa la Sudan Kusini lilipitisha marekebisho hayo Septema Mosi, na rais Kiir kuridhia siku inayofuata Septemba 2. Marekebisho hayo yanatenganisha uchaguzi wa Desemba 22…
Kambi ya Wahamiaji ya Ufukwe wa El Trampolin huko Ceuta,Hispania yaibuka tena
Ingawa hapo awali wahamiaji huko Ceuta,Hispania walihamishwa na kupelekwa maeneo maalum, ufukwe wa El Trampolin umejaa tena vibanda vingi vya muda. Inakadiriwa kuwa, baada ya wimbi la wahamiaji kuingia mwishoni mwa Julai, bado kuna wahamiaji kati ya 5,000 na 10,000 (wakiwemo watoto wasioandamana na wazazi) waliobakia Ceuta, na wengi wao wamejenga makazi ya muda kwenye…
Mkutano wa mifumo ya Chakula Afrika wafunguliwa Rwanda
Mkutano wa Mifumo ya Chakula Afrika umefunguliwa katika mji mkuu wa Rwanda, Kigali, na kuleta pamoja watunga sera, wakulima, wawekezaji, watafiti na wenzi wa maendeleo kwa lengo la kujadili njia za kufanyia mageuzi sekta ya chakula na kilimo katika bara la Afrika. Mkutano huo unajikita katika changamoto kubwa ikiwemo ufadhili, teknolojia, hasara baada ya mvuno,…
Watu 21 wafariki, 541 hawajulikani walipo baada ya maporomoko ya matope kuikumba forodha ya mpakani mkoani Xizang, China
Watu 21 wamethibitishwa kufariki na wengine 541 bado hawajulikani walipo hadi kufikia Jumatano mchana baada ya maporomoko ya matope kuikumba forodha ya Gyirong kwenye mpaka wa China na Nepal kusini magharibi mwa Mkoa wa Xizang Agosti 26. Habari zinasema waokoaji wamerejesha vipande 847 vya mali binafsi, mamlaka za mitaa zimepokea simu 876 kutoka kwa jamaa…
Teknolojia ya AI ya China yapata umaarufu nchini Kenya
Miundo ya Akili Bandia ya China (Al) inapata umaarufu miongoni mwa waendelezaji programu na makampuni ya teknolojia ya Kenya kutokana na sifa zake za gharama nafuu, utendaji wenye ushindani na kuwa Chanzo Huria, ikitoa chaguo la kuvutia kwa soko linalohitaji masuluhisho ya Akili Bandia yenye gharama nafuu na yanayokidhi mahitaji ya kienyeji. Uchambuzi wa hivi…
UM waonyesha wasiwasi kuhusu vurugu nchini Sudan
Umoja wa Mataifa umeonyesha wasiwasi kuhusu kuibuka kwa mapigano mapya nchini Sudan, ukisema mapigano hayo yanawaweka raia katika hatari kubwa na kuwafanya watu wengi zaidi kukimbia makazi yao. Mkoa wa Blue Nile umerekodi moja ya idadi kubwa ya watu wanaokimbia makazi yao, huku mamlaka za huko zikisema karibu watu 22,000 huenda wamekimbilia eneo la Gisan…
Handaki la kujikinga na mashambulizi ya anga huko Hangzhou yageuzwa kuwa “chumba chenye kiyoyozi cha asili”.
Watu wengi wanajiburudisha katika eneo la kupumzika lenye baridi huko Sipailou mjini Hangzhou mkoani Zhejiang,China. Eneo hilo limejengwa ndani ya handaki la kujikinga na mashambulizi ya anga, na ni kama “chumba chenye kiyoyozi cha asili” ambapo hali ya joto inadumishwa karibu nyuzijoto 25. Pia kumewekwa chumba cha kusoma vitabu,eneo la kucheza ping-pong, na viti 400…
Mgomo wa wafanyakazi wavuruga safari za anga nchini Kenya
Mgomo wa wafanyakazi wa anga ulioanza jumapili iliyopita nchini Kenya umesababisha shughuli za usafiri kuvurugika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) nchini humo kwa siku ya pili jana Jumatatu, huku maelfu ya wasafiri wakilalamikia kuahirishwa kwa safari zao au nyingine kukwama wasijue tarehe halisi ya safari zao. Jumapili iliyopita, Mamlaka ya…