China yazihimiza Iran na Marekani kurejea kwenye Makubaliano ya Maelewano ya Islamabad
Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi Jumatano alifanya mazungumzo na mwenzake wa Iran Seyyed Abbas Araghchi mjini Beijing. Wang amesema kuendelea kwa mapambano kati ya Marekani na Iran hakuendani na maslahi ya pamoja ya pande husika na jumuiya ya kimataifa. China inazihimiza Iran na Marekani zijizuie, kurejea kwenye Makubaliano ya Maelewano ya…
DR Congo na Rwanda zarejea Geneva kwa mazungumzo ya amani
Maafisa kutoka Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wamekutana Geneva tarehe 16 na 17 mwezi Septemba, wakishiriki kwenye kikao cha saba cha Mfumo wa Pamoja wa Uratibu wa Usalama (JSCM), huku nchi hizo mbili zikitafuta kuendeleza utekelezaji wa makubaliano yao ya amani yanayoungwa mkono na Marekani. Mazungumzo hayo yamewaleta pamoja wawakilishi wa Rwanda…
Marekani yaweka vikwazo vya viza kutokana na sera za Afrika Kusini kuhusu makabila na ardhi
Marekani imetangaza vikwazo vipya vya viza vinavyolenga raia fulani wa kigeni wanaohusishwa na sera za Afrika Kusini ambazo Marekani inasema zinabagua makabila madogo na zinaweza kuruhusu kunyang’anywa kwa ardhi bila fidia. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio alitangaza hatua hizo Jumanne, akisema kuwa serikali ya Afrika Kusini imeshindwa kushughulikia masuala yaliyowahi kuibuliwa…
Rais Ruto apongeza ushindi wa kihistoria wa Nairobi kuandaa Mashindano ya Riadha ya Dunia ya 2029
Rais wa Kenya William Ruto amepongeza hatua ya kuichagua Nairobi kuwa mwenyeji wa Mashindano ya Riadha ya Dunia ya 2029 akisema huo ni wakati wa kihistoria kwa Kenya na Afrika. Kenya itakuwa nchi ya kwanza ya Afrika kuwa mwenyeji wa Mashindano ya Riadha ya Dunia, ambalo ni tukio kuu la kimataifa la mchezo huo wa…
Mkutano wa Kilele wa Haidrojeni ya Kijani wa Afrika wafunguliwa huko Cape Town
Mkutano wa Kilele wa Haidrojeni ya Kijani Afrika wa 2026 umefunguliwa mjiniCape Town, ambapo Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ametoa wito wa kuharakisha utekelezaji na kuimarisha ushirikiano wa kiutendaji, ili kuubadilisha uwezekano wa haidrojeni ya kijani barani Afrika uwe ukuaji wa viwanda, usalama wa nishati, na maendeleo endelevu. Mkutano huo wa siku mbili umeshirikisha…
Tanzania yanufaika na Kongamano la BRI jijini Hong Kong baada ya kukutana na wawekezaji wa kimataifa
Tanzania imetumia Kongamano la Ukanda Mmoja Njia Moja lililofanyika Hong Kong kuanzia tarehe 9 hadi 10 Septemba 2026 kutangaza fursa za kimkakati za uwekezaji na kuimarisha mawasiliano na wawekezaji wa kimataifa pamoja na washirika watarajiwa wa kibiashara. Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), ikishirikiana na kampuni ya Opulence Business Solutions, iliratibu…
Lamine Yamal asema Mbappe ndiye mpinzani wake pekee katika tuzo ya Ballon d’Or
Lamine Yamal amesema mafanikio yake katika Kombe la Dunia akiwa na Hispania na kutwaa taji la LaLiga akiwa na Barcelona yanapaswa kumpa nafasi ya juu zaidi kuliko Kylian Mbappe wa Real Madrid katika kinyang’anyiro cha tuzo ya Ballon d’Or. Mshambuliaji wa Ufaransa, Mbappe, alikuwa mfungaji bora katika Kombe la Dunia pamoja na LaLiga na Ligi…
Kiwango cha maji cha Himalaya kufika kileleni, mamilioni ya maisha ya watu yako hatarini
Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti yaliyotolewa mwezi huu, kiwango cha barafu ya Himalaya kinakaribia kushuka ambapo inayeyuka haraka kuliko muongo mmoja uliopita, na kutishia usalama wa maji huku eneo hilo likikaribia “kilele chake cha maji” hadi katikati ya karne. Matokeo haya yanakuja baada ya kuanguka kwa barafu ya Himalaya mwishoni mwa Agosti kwenye mpaka…
Wizara ya Mambo ya Nje ya China: China na India zinapaswa kuwa washirika
Wizara ya Mambo ya Nje ya China imesema, rais Xi Jinping wa China na waziri mkuu wa India Bw. Narendra Modi wamekubaliana kwamba, China na India zinapaswa kuwa washirika, ambayo ni makubaliano muhimu zaidi kati ya viongozi hao wawili kuyafikia wakati wa mkutano wa 18 wa wakuu wa nchi za BRICS mjini New Delhi. Viongozi…
Rais Ramaphosa ataka BRICS kutetea ushirikiano na kusukuma mbele mageuzi ya usimamizi wa kimataifa
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ametoa wito kwa nchi za BRICS kuimarisha ushirikiano wa pande nyingi na kusukuma mbele mageuzi ya usimamizi wa kimataifa, akisisitiza sauti za Afrika na Dunia ya Kusini lazima ziakisi kikamilifu katika kuunda utaratibu wa kimataifa wa siku zijazo. Rais Ramaphosa ametoa wito huo katika kikao wa pembezoni mwa Mkutano…