Umoja wa Mataifa waunga mkono juhudi za kupambana na kipindupindu nchini Sudan
Ofisi ya Umoja wa Mataifa Inayoratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imesema, Umoja wa Mataifa na washirika wake wa kibinadamu wanaendelea kuunga mkono juhudi za kupambana na kipindupindu nchini Sudan na kutoa msaada muhimu kwa wahitaji licha ya changamoto za usalama. OCHA imesema kutokana na msaada wa Shirika la Afya Duniani (WHO), mamlaka za afya zimezindua…
Rais Xi Jinping atoa salamu za Siku ya Walimu, akihimiza kulea vijana wenye uwezo kwa uhuishaji wa taifa
Rais Xi Jinping wa China ametoa salamu kwa walimu na waelimishaji kote nchini kabla ya Siku ya Walimu inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 10 Septemba. Kwenye ujumbe wake wa pongezi, Rais Xi ametoa wito kwa walimu nchini kote kuimarisha umahiri na uwezo wao na kukuza kizazi kipya cha vijana kubeba majukumu yao ya kutimiza ustawi mpya…
Naibu waziri Mkuu wa China atoa wito wa uwazi na ushirikiano zaidi katika sekta ya huduma
Naibu Waziri Mkuu wa China, Bw. Ding Xuexiang, amesema kuendeleza biashara ya huduma na kuhimiza uwazi na ushirikiano katika sekta ya huduma si chaguo la China tu bali pia ni hitaji la dunia. Bw. Ding amesema kwenye Mkutano wa Kimataifa wa Biashara ya Huduma wa mwaka 2026 uliofanyika mjini Beijing, kuwa China imehimiza kikamilifu biashara…
Katibu mkuu wa UM ahimiza kurejesha mazungumzo kati ya Russia na Ukraine
Msemaji wa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Stéphane Dujarric amesema, katibu mkuu Bw. António Guterres anataka juhudi za kidiplomasia za hivi karibuni ziwezeshe kurejeshwa kwa mazungumzo kati ya Russia na Ukraine. Kwenye mkutano wa kawaida na wanahabari, Bw. Guterres amefurahia juhudi za kidiplomasia ikiwemo ziara ya mjumbe maalumu wa Marekani huko Moscow na…
Raia wa kigeni nchini Kenya wana siku 90 kuwa na vibali vya kazi
Kenya imewapa raia wa kigeni wanaoendesha biashara ndogo ndogo siku 90 za kuratibu hadhi yao ya uhamiaji, vibali vya kazi na leseni za biashara. Msemaji wa Ikulu ya Kenya Bw. Hussein Mohammed, amesema kazi hiyo itaratibiwa na balozi za raia wageni, na kuwapa fursa iliyo wazi na iliyopangwa ya kuratibu ukaazi wao na shughuli za…
Kundi la Hamas lasema lengo la Israel kusafisha kifusi huko Gaza ni kufuta “ushahidi wa uhalifu wa vita”
Kundi la Hamas lilitoa taarifa tarehe 7 Septemba likidai serikali ya Israel na jeshi lake wanajaribu kusafisha na kuhamisha kifusi huko Ukanda wa Gaza ili kuficha uhalifu waliowatendea watu wa Palestina. Taarifa hiyo imesema miili ya maelfu ya wahanga bado imezikwa chini ya kifusi, ambayo ni ushahidi wa moja kwa moja unaoweza kuthibitisha “uhalifu wa…
Mjumbe maalumu wa UM atahadharisha kuhusu hatari ya kuzorota kwa hali ya Yemen
Mjumbe maalumu wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia masuala ya Yemen Bw. Hans Grundberg tarehe 7 Septemba alitoa taarifa akisema kundi la Houthi hivi karibuni limefanya mashambulizi katika mistari kadhaa nchini Yemen, kusababisha kuongezeka kwa mapambano ya kisilaha, na kuongeza hatari ya kuzorotesha mgogoro wa nchini humo, hali inayoleta wasiwasi mkubwa. Taarifa imesema…
Serikali ya Tanzania yapanga kutumia teknolojia kukuza uchumi wa bluu
Serikali ya Tanzania inaendelea kuimarisha matumizi ya teknolojia za kidijitali, mifumo ya kisasa ya usimamizi wa bandari na biashara, pamoja na matumizi ya taarifa za kisayansi katika kufanya maamuzi kwa lengo la kuimarisha maendeleo ya uchumi wa bluu nchini. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bw.Hamadi Masauni, amesema hayo wakati…
Afisa wa UM atembelea DRC kutathmini mwitikio wa janga la Ebola
Ofisi ya Uratibu wa Mambo ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) imesema janga la Ebola linaloendelea kuenea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) limesababisha vifo zaidi ya 3,200. Mratibu wa OCHA Bw. Damien Mama ameanza ziara ya yake ya siku nne katika jimbo la Kivu Kaskazini nchini DRC kuanzia tarehe 8 ili…
Nchi kuu zinazozalisha mafuta za “OPEC+” zaamua kudumisha kiwango cha uzalishaji Oktoba
Shirika la Nchi Zinazozalisha Mafuta (OPEC) lilitoa taarifa tarehe 6 Septemba likisema nchi saba wanachama za “OPEC+” zimeamua kudumisha kiwango cha uzalishaji wa mafuta ghafi mwezi Oktoba, sawa na kilekile cha Septemba, huku zikisisitiza tena kulinda utulivu wa soko. Wawakilishi kutoka Saudi Arabia, Russia, Iraq, Kuwait, Kazakhstan, Algeria na Oman walifanya mkutano kwa njia ya…