Rais Ramaphosa ataka BRICS kutetea ushirikiano na kusukuma mbele mageuzi ya usimamizi wa kimataifa
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ametoa wito kwa nchi za BRICS kuimarisha ushirikiano wa pande nyingi na kusukuma mbele mageuzi ya usimamizi wa kimataifa, akisisitiza sauti za Afrika na Dunia ya Kusini lazima ziakisi kikamilifu katika kuunda utaratibu wa kimataifa wa siku zijazo. Rais Ramaphosa ametoa wito huo katika kikao wa pembezoni mwa Mkutano…
Gharama za bidhaa zapanda nchini Somalia kutokana na usumbufu wa usafirishaji katika Bahari ya Sham
Bei ya bidhaa imepanda nchini Somalia na kuongeza wasiwasi wa usalama baharini kutokana na mashambulizi ya Wahouthi kuvuruga usafirishaji kupitia Mlangobahari wa Bab al-Mandab. Gharama ya gesi ya kupikia kwa chupa ya kilo 10 imepanda kutoka takriban $25 hadi $40, ambapo bei ya mafuta imeongezeka mara mbili hadi $1.50 kwa lita. Bei za chakula pia…
Mwenge wa Olimpiki wawasili Senegal kwa ajili ya Michezo ya Vijana, tukio la kwanza la Olimpiki Afrika
Mwenge wa Olimpiki ulipokelewa kwa muziki na ngoma katika mji mkuu wa Senegal siku ya Jumamosi, huku matembezi ya wanawake 100 yakiashiria kuanza kuhesabu muda kuelekea siku ya tukio la kwanza la michezo ya Olimpiki kufanyika barani Afrika, yaani Michezo ya Olimpiki ya Vijana. Zaidi ya watu mia moja walikusanyika katika eneo la Place du…
Uganda yatangaza timu ya wachezaji 28 kwa AFCON ya 2027
Kocha mkuu wa timu ya Uganda Paul Put ametangaza timu ya wachezaji 28 kwa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) la 2027. Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka la Afrika (CAF), michuano ya hatua ya makundi itaanza mwezi huu, na kuendelea hadi mwezi Machi mwakani. Put alitangaza timu ya wachezaji Alhamisi kabla ya mechi za…
Kenya yaanzisha mpango wa kukabiliana na El Nino ili kulinda mifugo
Kenya imeanzisha mpango wa hatua za mapema kukabiliana na athari za El Nino kwa sekta ya mifugo Alhamisi wiki hii, ukiwa na thamani ya shilingi za Kenya bilioni 2.1 (takriban dola za kimarekani milioni 16.2). Waziri wa maendeleo ya mifugo na kilimo Bw. Mutahi Kagwe amesisitiza ahadi ya serikali ya kulinda uchumi wa mifugo kwa…
Watu 26 wafariki katika ajali ya moto shuleni mashariki mwa DRC
Vyombo vya habari nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) vimeripoti kuwa, wanafunzi 26 wamefariki na wengine wengi kujeruhiwa katika ajali ya moto mkubwa uliozuka jana huko Bukavu, mji mkuu wa mkoa wa Kivu Kusini, mashariki mwa nchi hiyo. Ripoti hizo zinasema, miili ya marehemu imepelekwa hospitali za eneo hilo, na idadi kamili ya watu…
Umoja wa Mataifa waunga mkono juhudi za kupambana na kipindupindu nchini Sudan
Ofisi ya Umoja wa Mataifa Inayoratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imesema, Umoja wa Mataifa na washirika wake wa kibinadamu wanaendelea kuunga mkono juhudi za kupambana na kipindupindu nchini Sudan na kutoa msaada muhimu kwa wahitaji licha ya changamoto za usalama. OCHA imesema kutokana na msaada wa Shirika la Afya Duniani (WHO), mamlaka za afya zimezindua…
Rais Xi Jinping atoa salamu za Siku ya Walimu, akihimiza kulea vijana wenye uwezo kwa uhuishaji wa taifa
Rais Xi Jinping wa China ametoa salamu kwa walimu na waelimishaji kote nchini kabla ya Siku ya Walimu inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 10 Septemba. Kwenye ujumbe wake wa pongezi, Rais Xi ametoa wito kwa walimu nchini kote kuimarisha umahiri na uwezo wao na kukuza kizazi kipya cha vijana kubeba majukumu yao ya kutimiza ustawi mpya…
Naibu waziri Mkuu wa China atoa wito wa uwazi na ushirikiano zaidi katika sekta ya huduma
Naibu Waziri Mkuu wa China, Bw. Ding Xuexiang, amesema kuendeleza biashara ya huduma na kuhimiza uwazi na ushirikiano katika sekta ya huduma si chaguo la China tu bali pia ni hitaji la dunia. Bw. Ding amesema kwenye Mkutano wa Kimataifa wa Biashara ya Huduma wa mwaka 2026 uliofanyika mjini Beijing, kuwa China imehimiza kikamilifu biashara…
Katibu mkuu wa UM ahimiza kurejesha mazungumzo kati ya Russia na Ukraine
Msemaji wa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Stéphane Dujarric amesema, katibu mkuu Bw. António Guterres anataka juhudi za kidiplomasia za hivi karibuni ziwezeshe kurejeshwa kwa mazungumzo kati ya Russia na Ukraine. Kwenye mkutano wa kawaida na wanahabari, Bw. Guterres amefurahia juhudi za kidiplomasia ikiwemo ziara ya mjumbe maalumu wa Marekani huko Moscow na…