Mkutano wa Kilele wa Haidrojeni ya Kijani wa Afrika wafunguliwa huko Cape Town

Mkutano wa Kilele wa Haidrojeni ya Kijani Afrika wa 2026 umefunguliwa mjiniCape Town, ambapo Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ametoa wito wa kuharakisha utekelezaji na kuimarisha ushirikiano wa kiutendaji, ili kuubadilisha uwezekano wa haidrojeni ya kijani barani Afrika uwe ukuaji wa viwanda, usalama wa nishati, na maendeleo endelevu. Mkutano huo wa siku mbili umeshirikisha…

Read More

Tanzania yanufaika na Kongamano la BRI jijini Hong Kong baada ya kukutana na wawekezaji wa kimataifa

Tanzania imetumia Kongamano la Ukanda Mmoja Njia Moja lililofanyika Hong Kong kuanzia tarehe 9 hadi 10 Septemba 2026 kutangaza fursa za kimkakati za uwekezaji na kuimarisha mawasiliano na wawekezaji wa kimataifa pamoja na washirika watarajiwa wa kibiashara. Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), ikishirikiana na kampuni ya Opulence Business Solutions, iliratibu…

Read More

Kiwango cha maji cha Himalaya kufika kileleni, mamilioni ya maisha ya watu yako hatarini

Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti yaliyotolewa mwezi huu, kiwango cha barafu ya Himalaya kinakaribia kushuka ambapo inayeyuka haraka kuliko muongo mmoja uliopita, na kutishia usalama wa maji huku eneo hilo likikaribia “kilele chake cha maji” hadi katikati ya karne. Matokeo haya yanakuja baada ya kuanguka kwa barafu ya Himalaya mwishoni mwa Agosti kwenye mpaka…

Read More

Rais Ramaphosa ataka BRICS kutetea ushirikiano na kusukuma mbele mageuzi ya usimamizi wa kimataifa

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ametoa wito kwa nchi za BRICS kuimarisha ushirikiano wa pande nyingi na kusukuma mbele mageuzi ya usimamizi wa kimataifa, akisisitiza sauti za Afrika na Dunia ya Kusini lazima ziakisi kikamilifu katika kuunda utaratibu wa kimataifa wa siku zijazo. Rais Ramaphosa ametoa wito huo katika kikao wa pembezoni mwa Mkutano…

Read More

Gharama za bidhaa zapanda nchini Somalia kutokana na usumbufu wa usafirishaji katika Bahari ya Sham

Bei ya bidhaa imepanda nchini Somalia na kuongeza wasiwasi wa usalama baharini kutokana na mashambulizi ya Wahouthi kuvuruga usafirishaji kupitia Mlangobahari wa Bab al-Mandab. Gharama ya gesi ya kupikia kwa chupa ya kilo 10 imepanda kutoka takriban $25 hadi $40, ambapo bei ya mafuta imeongezeka mara mbili hadi $1.50 kwa lita. Bei za chakula pia…

Read More

Mwenge wa Olimpiki wawasili Senegal kwa ajili ya Michezo ya Vijana, tukio la kwanza la Olimpiki Afrika

Mwenge wa Olimpiki ulipokelewa kwa muziki na ngoma katika mji mkuu wa Senegal siku ya Jumamosi, huku matembezi ya wanawake 100 yakiashiria kuanza kuhesabu muda kuelekea siku ya tukio la kwanza la michezo ya Olimpiki kufanyika barani Afrika, yaani Michezo ya Olimpiki ya Vijana. Zaidi ya watu mia moja walikusanyika katika eneo la Place du…

Read More

LEOFM

Maisha TV
Live
Tap to listen live