OpenAI yaibua wasiwasi kuhusu tabia mpya ya Akili Bandia na kuahidi kuifuatilia kwa karibu zaidi
OpenAI imetoa ripoti sita kuhusu tabia “zisizotarajiwa au za kutia wasiwasi” katika mifumo ya akili bandia (AI), huku mjadala kuhusu usalama wa teknolojia hiyo ukizidi kushika kasi. Kampuni hiyo ya Akili bandia pia Jumatano ilitangaza kuwa inaleta mfumo mpya wa kufuatilia, kuchunguza na kuweka wazi matukio ya kile ilichokiita “kutokwenda sambamba na malengo yaliyokusudiwa” yakiwemo…
Baraza Kuu la UM lamruhusu Abbas kushiriki katika mjadala wa jumla kupitia video
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio la kumruhusu Rais wa Palestina Mahmoud Abbas kushiriki katika mjadala wa jumla wa mwaka huu kupitia video, kufuatia hatua ya Marekani ya kumnyima viza. Azimio hilo lililopitishwa kwa kura 152 za ndiyo, 3 za hapana na 4 zisizopigwa, limeamua kuwa Palestina inaweza kuwasilisha taarifa ya Abbas iliyorekodiwa…
Waziri wa Mambo ya Nje wa China azungumza na Rubio kwa njia ya simu kuhusu maingiliano ya ngazi ya juu
Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi jana alifanya mazungumzo na mwenzake wa Marekani Marco Rubio kwa njia ya simu kuhusu maingiliano ya ngazi ya juu kati ya nchi hizo mbili. Wakati wa mazungumzo yao, Bw. Wang alibainisha kuwa diplomasia ya wakuu wa nchi ndiyo nguzo ya uhusiano kati ya China na Marekani,…
China yazihimiza Iran na Marekani kurejea kwenye Makubaliano ya Maelewano ya Islamabad
Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi Jumatano alifanya mazungumzo na mwenzake wa Iran Seyyed Abbas Araghchi mjini Beijing. Wang amesema kuendelea kwa mapambano kati ya Marekani na Iran hakuendani na maslahi ya pamoja ya pande husika na jumuiya ya kimataifa. China inazihimiza Iran na Marekani zijizuie, kurejea kwenye Makubaliano ya Maelewano ya…
DR Congo na Rwanda zarejea Geneva kwa mazungumzo ya amani
Maafisa kutoka Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wamekutana Geneva tarehe 16 na 17 mwezi Septemba, wakishiriki kwenye kikao cha saba cha Mfumo wa Pamoja wa Uratibu wa Usalama (JSCM), huku nchi hizo mbili zikitafuta kuendeleza utekelezaji wa makubaliano yao ya amani yanayoungwa mkono na Marekani. Mazungumzo hayo yamewaleta pamoja wawakilishi wa Rwanda…
Marekani yaweka vikwazo vya viza kutokana na sera za Afrika Kusini kuhusu makabila na ardhi
Marekani imetangaza vikwazo vipya vya viza vinavyolenga raia fulani wa kigeni wanaohusishwa na sera za Afrika Kusini ambazo Marekani inasema zinabagua makabila madogo na zinaweza kuruhusu kunyang’anywa kwa ardhi bila fidia. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio alitangaza hatua hizo Jumanne, akisema kuwa serikali ya Afrika Kusini imeshindwa kushughulikia masuala yaliyowahi kuibuliwa…
Rais Ruto apongeza ushindi wa kihistoria wa Nairobi kuandaa Mashindano ya Riadha ya Dunia ya 2029
Rais wa Kenya William Ruto amepongeza hatua ya kuichagua Nairobi kuwa mwenyeji wa Mashindano ya Riadha ya Dunia ya 2029 akisema huo ni wakati wa kihistoria kwa Kenya na Afrika. Kenya itakuwa nchi ya kwanza ya Afrika kuwa mwenyeji wa Mashindano ya Riadha ya Dunia, ambalo ni tukio kuu la kimataifa la mchezo huo wa…
Mkutano wa Kilele wa Haidrojeni ya Kijani wa Afrika wafunguliwa huko Cape Town
Mkutano wa Kilele wa Haidrojeni ya Kijani Afrika wa 2026 umefunguliwa mjiniCape Town, ambapo Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ametoa wito wa kuharakisha utekelezaji na kuimarisha ushirikiano wa kiutendaji, ili kuubadilisha uwezekano wa haidrojeni ya kijani barani Afrika uwe ukuaji wa viwanda, usalama wa nishati, na maendeleo endelevu. Mkutano huo wa siku mbili umeshirikisha…
Tanzania yanufaika na Kongamano la BRI jijini Hong Kong baada ya kukutana na wawekezaji wa kimataifa
Tanzania imetumia Kongamano la Ukanda Mmoja Njia Moja lililofanyika Hong Kong kuanzia tarehe 9 hadi 10 Septemba 2026 kutangaza fursa za kimkakati za uwekezaji na kuimarisha mawasiliano na wawekezaji wa kimataifa pamoja na washirika watarajiwa wa kibiashara. Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), ikishirikiana na kampuni ya Opulence Business Solutions, iliratibu…
Lamine Yamal asema Mbappe ndiye mpinzani wake pekee katika tuzo ya Ballon d’Or
Lamine Yamal amesema mafanikio yake katika Kombe la Dunia akiwa na Hispania na kutwaa taji la LaLiga akiwa na Barcelona yanapaswa kumpa nafasi ya juu zaidi kuliko Kylian Mbappe wa Real Madrid katika kinyang’anyiro cha tuzo ya Ballon d’Or. Mshambuliaji wa Ufaransa, Mbappe, alikuwa mfungaji bora katika Kombe la Dunia pamoja na LaLiga na Ligi…